Back to Languages

Swahili - Chapter 1

Translation by Ali Muhsin Al Barwani

Verse 1

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

Verse 2

Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote

Verse 3

Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu

Verse 4

Mwenye Kumiliki Siku ya Malipo

Verse 5

Wewe tu tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada

Verse 6

Tuongoe njia iliyo nyooka

Verse 7

Njia ya ulio waneemesha, siyo ya walio kasirikiwa, wala walio potea