Back to Languages
Swahili - Chapter 1
Translation by Ali Muhsin Al Barwani
Verse 1
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
Verse 2
Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote
Verse 3
Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu
Verse 4
Mwenye Kumiliki Siku ya Malipo
Verse 5
Wewe tu tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada
Verse 6
Tuongoe njia iliyo nyooka
Verse 7
Njia ya ulio waneemesha, siyo ya walio kasirikiwa, wala walio potea