Back to Languages
Swahili - Chapter 55
Translation by Ali Muhsin Al Barwani
Verse 1
Arrah'man, Mwingi wa Rehema
Verse 2
Amefundisha Qur'ani
Verse 3
Amemuumba mwanaadamu
Verse 4
Akamfundisha kubaini
Verse 5
Jua na mwezi huenda kwa hisabu
Verse 6
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea
Verse 7
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani
Verse 8
Ili msidhulumu katika mizani
Verse 9
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani
Verse 10
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe
Verse 11
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba
Verse 12
Na nafaka zenye makapi, na rehani
Verse 13
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 14
Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo
Verse 15
Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto
Verse 16
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 17
Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili
Verse 18
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 19
Anaziendesha bahari mbili zikutane
Verse 20
Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane
Verse 21
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 22
Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani
Verse 23
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 24
Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima
Verse 25
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 26
Kila kilioko juu yake kitatoweka
Verse 27
Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu
Verse 28
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 29
Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo
Verse 30
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 31
Tutakuhisabuni enyi makundi mawili
Verse 32
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 33
Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka
Verse 34
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 35
Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda
Verse 36
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 37
Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta
Verse 38
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 39
Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini
Verse 40
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 41
Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu
Verse 42
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 43
Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha
Verse 44
Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka
Verse 45
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 46
Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili
Verse 47
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 48
Bustani zenye matawi yaliyo tanda
Verse 49
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 50
Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita
Verse 51
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 52
Humo katika kila matunda zimo namna mbili
Verse 53
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 54
Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu
Verse 55
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 56
Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini
Verse 57
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 58
Kama kwamba wao ni yakuti na marijani
Verse 59
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 60
Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani
Verse 61
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 62
Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili
Verse 63
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 64
Za kijani kibivu
Verse 65
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 66
Na chemchem mbili zinazo furika
Verse 67
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 68
Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga
Verse 69
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 70
Humo wamo wanawake wema wazuri
Verse 71
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 72
Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema
Verse 73
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 74
Hajawagusa mtu wala jini kabla yao
Verse 75
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 76
Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri
Verse 77
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Verse 78
Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu