Back to Languages

Swahili - Chapter 55

Translation by Ali Muhsin Al Barwani

Verse 1

Arrah'man, Mwingi wa Rehema

Verse 2

Amefundisha Qur'ani

Verse 3

Amemuumba mwanaadamu

Verse 4

Akamfundisha kubaini

Verse 5

Jua na mwezi huenda kwa hisabu

Verse 6

Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea

Verse 7

Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani

Verse 8

Ili msidhulumu katika mizani

Verse 9

Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani

Verse 10

Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe

Verse 11

Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba

Verse 12

Na nafaka zenye makapi, na rehani

Verse 13

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 14

Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo

Verse 15

Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto

Verse 16

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 17

Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili

Verse 18

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 19

Anaziendesha bahari mbili zikutane

Verse 20

Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane

Verse 21

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 22

Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani

Verse 23

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 24

Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima

Verse 25

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 26

Kila kilioko juu yake kitatoweka

Verse 27

Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu

Verse 28

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 29

Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo

Verse 30

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 31

Tutakuhisabuni enyi makundi mawili

Verse 32

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 33

Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka

Verse 34

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 35

Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda

Verse 36

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 37

Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta

Verse 38

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 39

Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini

Verse 40

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 41

Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu

Verse 42

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 43

Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha

Verse 44

Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka

Verse 45

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 46

Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili

Verse 47

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 48

Bustani zenye matawi yaliyo tanda

Verse 49

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 50

Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita

Verse 51

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 52

Humo katika kila matunda zimo namna mbili

Verse 53

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 54

Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu

Verse 55

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 56

Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini

Verse 57

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 58

Kama kwamba wao ni yakuti na marijani

Verse 59

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 60

Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani

Verse 61

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 62

Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili

Verse 63

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 64

Za kijani kibivu

Verse 65

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 66

Na chemchem mbili zinazo furika

Verse 67

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 68

Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga

Verse 69

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 70

Humo wamo wanawake wema wazuri

Verse 71

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 72

Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema

Verse 73

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 74

Hajawagusa mtu wala jini kabla yao

Verse 75

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 76

Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri

Verse 77

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

Verse 78

Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu