Back to Languages

    Swahili - Chapter 69

    Translation by Ali Muhsin Al Barwani

    Verse 1

    Tukio la haki

    Verse 2

    Nini hilo Tukio la haki

    Verse 3

    Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki

    Verse 4

    Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha

    Verse 5

    Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno

    Verse 6

    Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika

    Verse 7

    Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani

    Verse 8

    Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki

    Verse 9

    Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia

    Verse 10

    Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu

    Verse 11

    Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina

    Verse 12

    Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi

    Verse 13

    Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu

    Verse 14

    Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja

    Verse 15

    Siku hiyo ndio Tukio litatukia

    Verse 16

    Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa

    Verse 17

    Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi

    Verse 18

    Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu

    Verse 19

    Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu

    Verse 20

    Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu

    Verse 21

    Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza

    Verse 22

    Katika Bustani ya juu

    Verse 23

    Matunda yake yakaribu

    Verse 24

    Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita

    Verse 25

    Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu

    Verse 26

    Wala nisingeli jua nini hisabu yangu

    Verse 27

    Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa

    Verse 28

    Mali yangu hayakunifaa kitu

    Verse 29

    Madaraka yangu yamenipotea

    Verse 30

    (Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu

    Verse 31

    Kisha mtupeni Motoni

    Verse 32

    Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini

    Verse 33

    Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu

    Verse 34

    Wala hahimizi kulisha masikini

    Verse 35

    Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu

    Verse 36

    Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni

    Verse 37

    Chakula hicho hawakili ila wakosefu

    Verse 38

    Basi naapa kwa mnavyo viona

    Verse 39

    Na msivyo viona

    Verse 40

    Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima

    Verse 41

    Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini

    Verse 42

    Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka

    Verse 43

    Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote

    Verse 44

    Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu

    Verse 45

    Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia

    Verse 46

    Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo

    Verse 47

    Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia

    Verse 48

    Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu

    Verse 49

    Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha

    Verse 50

    Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa

    Verse 51

    Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini

    Verse 52

    Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu