Back to Languages
Swahili - Chapter 75
Translation by Ali Muhsin Al Barwani
Verse 1
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama
Verse 2
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu
Verse 3
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake
Verse 4
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake
Verse 5
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake
Verse 6
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama
Verse 7
Basi jicho litapo dawaa
Verse 8
Na mwezi utapo patwa
Verse 9
Na likakusanywa jua na mwezi
Verse 10
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio
Verse 11
La! Hapana pa kukimbilia
Verse 12
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu
Verse 13
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha
Verse 14
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake
Verse 15
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru
Verse 16
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka
Verse 17
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha
Verse 18
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake
Verse 19
Kisha ni juu yetu kuubainisha
Verse 20
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani
Verse 21
Na mnaacha maisha ya Akhera
Verse 22
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara
Verse 23
Zinamwangallia Mola wao Mlezi
Verse 24
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana
Verse 25
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo
Verse 26
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo
Verse 27
Na pakasemwa: Nani wa kumganga
Verse 28
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki
Verse 29
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi
Verse 30
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi
Verse 31
Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali
Verse 32
Bali alikanusha, na akageuka
Verse 33
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao
Verse 34
Ole wako, ole wako
Verse 35
Kisha Ole wako, ole wako
Verse 36
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure
Verse 37
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa
Verse 38
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo
Verse 39
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke
Verse 40
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu