Back to Languages

    Swahili - Chapter 77

    Translation by Ali Muhsin Al Barwani

    Verse 1

    Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole

    Verse 2

    Na zinazo vuma kwa kasi

    Verse 3

    Na zikaeneza maeneo yote

    Verse 4

    Na zinazo farikisha zikatawanya

    Verse 5

    Na zinazo peleka mawaidha

    Verse 6

    Kwa kuudhuru au kuonya

    Verse 7

    Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa

    Verse 8

    Wakati nyota zitakapo futwa

    Verse 9

    Na mbingu zitakapo pasuliwa

    Verse 10

    Na milima itakapo peperushwa

    Verse 11

    Na Mitume watakapo wekewa wakati wao

    Verse 12

    Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo

    Verse 13

    Kwa siku ya kupambanua

    Verse 14

    Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini

    Verse 15

    Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha

    Verse 16

    Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia

    Verse 17

    Kisha tukawafuatilizia walio fuatia

    Verse 18

    Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu

    Verse 19

    Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha

    Verse 20

    Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa

    Verse 21

    Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti

    Verse 22

    Mpaka muda maalumu

    Verse 23

    Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria

    Verse 24

    Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha

    Verse 25

    Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya

    Verse 26

    Walio hai na maiti

    Verse 27

    Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu

    Verse 28

    Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha

    Verse 29

    Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha

    Verse 30

    Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu

    Verse 31

    Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako

    Verse 32

    Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba

    Verse 33

    Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano

    Verse 34

    Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha

    Verse 35

    Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu

    Verse 36

    Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru

    Verse 37

    Ole wao siku hiyo hao walio kanusha

    Verse 38

    Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia

    Verse 39

    Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi

    Verse 40

    Ole wao siku hiyo hao walio kanusha

    Verse 41

    Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem

    Verse 42

    Na matunda wanayo yapenda

    Verse 43

    Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda

    Verse 44

    Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema

    Verse 45

    Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha

    Verse 46

    Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu

    Verse 47

    Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha

    Verse 48

    Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami

    Verse 49

    Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha

    Verse 50

    Basi maneno gani baada ya haya watayaamini