Back to Languages
Swahili - Chapter 81
Translation by Ali Muhsin Al Barwani
Verse 1
Jua litakapo kunjwa
Verse 2
Na nyota zikazimwa
Verse 3
Na milima ikaondolewa
Verse 4
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe
Verse 5
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa
Verse 6
Na bahari zikawaka moto
Verse 7
Na nafsi zikaunganishwa
Verse 8
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa
Verse 9
Kwa kosa gani aliuliwa
Verse 10
Na madaftari yatakapo enezwa
Verse 11
Na mbingu itapo tanduliwa
Verse 12
Na Jahannamu itapo chochewa
Verse 13
Na Pepo ikasogezwa
Verse 14
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha
Verse 15
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma
Verse 16
Zinazo kwenda, kisha zikajificha
Verse 17
Na kwa usiku unapo pungua
Verse 18
Na kwa asubuhi inapo pambazuka
Verse 19
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu
Verse 20
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi
Verse 21
Anaye t'iiwa, tena muaminifu
Verse 22
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu
Verse 23
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi
Verse 24
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu
Verse 25
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni
Verse 26
Basi mnakwenda wapi
Verse 27
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote
Verse 28
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa
Verse 29
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote