Back to Languages

Swahili - Chapter 97

Translation by Ali Muhsin Al Barwani

Verse 1

Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'ani katika Laylatul Qadri, Usiku wa Cheo Kitukufu

Verse 2

Na nini kitacho kujuulisha nini Laylatul Qadri

Verse 3

Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu

Verse 4

Huteremka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa kila jambo

Verse 5

Amani usiku huo mpaka mapambazuko ya alfajiri